Kama
ni mali asili zipo kibao, kama ni madini yapo kibao, mpaka tunawapa wageni kwa
kiwango kidogo sawa na bure, kama ni maziwa yapo kibao , kama ni ardhi iko
kubwa jamani na bado hadi sasa Tanzania ipo katika nchi zinazoongoza kwa umasikini
barani Africa na duniani. Nashindwa kuelewa hivi ni kwanini umasikini unazidi
kuenea katika nchi yetu pamoja na vyote tulivyo navyo.
Maeneo
ya vijijini mkulima anaamka kabla jogoo hajawika ili tu awahi shambani . kila
siku mvua yake jua lake ili mradi tu apate kitu kidogo, ili mkono uende
kinywani . Upo mtizamo kwamba sababu ya kuendelea kwa umasikini wetu ni kwa
kuwa watanzania tunamiliki mali lakini hazina urasmi yamkini ya kutuwezesha
kupata mikopo katika taasisi mbalimbali za kiserikali ,na ndio maana ukaja
mkakati wa kurasimisha mali hizo kama harakati mojawapo ya kupambana na ufukara
nchini kupitia mikopo hiyo
Katika
harakati za kusaidia kuondokana na umaskini tumehimizwa kuifuata fursa yoyote
inapotokea mfano kununua hisa katika
mashirika tofauti nchini swali ni je mwananchi anayeishi kijijini ana elimu
gani kuhusu swala zima la hisa? Umasikini umeendelea kuenea nchini kwetu katika
sekta mbalimbali. Tatizo jingine ni ukosefu wa ajira kwa vijana wengi nchini ila kimantiki hili halikupaswa
kuwepo kutokana na sayansi na teknolojia kuenea ambapo matumizi ya maarifa
yameongezeka na pia kumekuwa na urahisishwaji wa kazi mbalimbali tofauti na
kipindi cha analojia. Hivyo inawezekana kuwa tatizo sio ajira ila tatizo ni
vijana wengi nchini hawana elimu .
Kuna
sekta kama kilimo lakini vijana wengi wanaikimbia na kusema kuwa wazee ndio
wanapaswa kufanya kazi za kilimo ,pia tumeona serikalini ufisadi na wizi
umetawala kile ambacho walipaswa kupewa wananchi kwa manufaa yao wenyewe
kinachukuliwa na watu walioko na madaraka. Hiyo inapelekea watu na nchi
kuendelea kuwa masikini.
Umefikia
wakati sasa tujishughulishe ili kuondoa na kumaliza umasikini nchini,
tuwashughulikie wezi wote mafisadi na hata wale waomba rushwa katika sekta
mbalimbali mfano sekta ya afya sekta ya kilimo, sekta ya elimu,miundombinu na usafiri nk ili tuweze kulinusuru taifa kutokana na
umasikini. Pia vijana wafanye kazi kwa bidii na kutumia rasilimali tulizonazo
ili tuweze kuliletea mapato taifa letu na wananchi kwa ujumla.